Translations:Forgiving Step by Step/2/sw

Kwa mara nyingi watu hujiepusha na hali kama hiyo na wanajenga kuta na vizuizi ili kujichunga. Kinachofuata hatuwezi kuhusiana na mtu yeyote kwa undani na tunajipata tumejitenga. Badala ya kujishughulisha na kutafuta suluhisho kwa jambo fulani tunasalia katika hali ya hasira, kutosameheana na vile vile kulipizana kisasi. Katika hali hii mawazo yetu yanasalia kwa mabaya tuliyotendewa na kuwaza sana ambavyo tumekosewa na wenzetu.