Translations:Forgiving Step by Step/4/sw

Kuna njia moja tu ya kuepukana na huu mviringo wa mabaya ambayo ni msamaha. Msamaha sio jambo la urahisi hasa kama umeumizwa na kusalia na machungu. La muhimu ni kwamba tusahau mabaya na tujiondoe kwa machungu tuliotendewa awali ili tusiwe wafungwa wa yaliyopita. Japo ni vigumu kusahau tuliyotendewa na tunaweza kujaribu kujipa suluhisho la muda na kukandamiza fikira zinazotuumiza. Mwenyezi Mungu ana nia ya kutupa uhuru, tuwe na uhuru kutoka kwa machungu, hasira, kulipiza kisasi na mengine mengi.