Translations:Forgiving Step by Step/6/sw
Msamaha ni kukata kauli kuachana na hasira na hisia zote mbaya dhidi ya wale waliotuumiza. Ni kuamua kumkabidhi aliyetukera katika mikono ya mwenyezi Mungu. Badala ya kuhukumu na kutaka kuwa muamuzi wa mabaya niliyotendewa, ni kuacha mwenyezi aamue atakalotenda na muasi wangu. Zaidi, ni kuamini kuwa Mungu ana hekima ya kuamua vyema kati yako na aliyekosa. Pia ni kukoma kuhesabu makosa uliyotendewa kwani maji yakimwagika hayazoleki, na kufungua ukurasa mpya kwa amani kati yenu.